Iran Yadai Kuilipua Meli Kubwa ya Ndege za Kivita ya Marekani (Aircraft Carrier)!
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) linasema limefanya shambulizi la makombora ya masafa marefu (ballistic missiles) dhidi ya Meli Kubwa ya Kubeba Ndege za Kivita ya Marekani pamoja na Meli ya Kivita ya Ulinzi (Destroyer) katika Bahari ya Arabu. Kwa mujibu wa IRGC, meli zote mbili zilipata uharibifu na kulazimika kurudi nyuma na kuondoka kwenye eneo la mapambano. Hata hivyo, madai haya bado hayajathibitishwa na vyanzo huru. Tehran imeonya kuwa itafanya mashambulizi zaidi dhidi ya meli za kivita za Marekani zinazofanya operesheni zake katika ukanda huo ikiwa mzingiro wa baharini (naval blockade) utaendelea, hatua inayoashiria uwezekano wa kupanda zaidi kwa mvutano. Tukio hili linaloripotiwa linaweza kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na matukio yanayodaiwa kuifanya Marekani kulipiza kisasi kwa kushambulia meli tatu za mafuta za Iran hapo awali. Wakati mivutano ikizidi kupanda kote kanda hiyo, mapambano kati ya Washington na Tehran yanaonekana kuingia katika hatu...